MigogoroMashariki ya Kati
Israel yatuhumiwa kutaka kuunyakua Ukingo wa Magharibi
25 Februari 2025Matangazo
Katika operesheni hiyo pana ya kijeshi inayoendelea hasa kwenye kambi ya wakimbizi ya Jenin, vikosi vya Israel vimeharibu mitaa, kichimbua barabara na miundombinu mingine kwa madai ya kuusambaratisha mtandao wa magaidi.
Mnamo siku ya Jumapili Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz alisema wanawajeshi wa nchi hiyo watabakia eneo la Ukingo wa Magharibi kwa muda mrefu hasa kwenye miji ya Jenin, Tulkarem na Nur Shams.
Kundi la Wanamgambo wa Kipalestina la Islamic Jihad limesema mipango hiyo inayombatana na kufukuzwa kwa idadi kubwa ya watu ni dalili za nia ya Israel kulichukua kikamilifu eneo hilo inalolikalia kinyume cha sheria ya kimataifa tangu mwaka 1967.