Israel yaunga mkono mpango wa Marekani wa kutoa misaada Gaza
11 Mei 2025Saar ameupongeza mpango huo uliowasilishwa na balozi wa Marekani kwa Israel Mike Huckabee akieleza kuwa utaruhusu misaada iwafikie wakaazi wa Gaza moja kwa moja bila kuangukia mikononi mwa wanamgambo wa Hamas.
Akizungumza Jumapili 11.05.2025 mjini Jerusalem Waziri huyo wa mambo ya nje wa Israel amefafanua kuwa chini ya mpango huo wanajeshi wa Israel hawatashiriki kugawa misaada bali watahakikisha unawafikia raia.
Soma zaidi: Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaonya kuhusu usambazaji misaada Gaza
Balozi wa Marekani nchini Israel aliuwasilisha mpango huo Ijumaa, siku moja baada ya Wizara ya Mambo ya nje ya Marekani kusema utasaidia kutoa misaada ya kiutu kwenye Ukanda wa Gaza ulioathiriwa vibaya na vita. Hata hivyo mpango huo unakabiliwa na ukosoaji kwa madai kuwa unautenga Umoja wa Mataifa na mashirika ya misaada yaliyo kwenye Ukanda huo.