Israel yanasa kombora lililorushwa na Wahouthi wa Yemen
27 Aprili 2025Matangazo
Jeshi hilo la Israel limesema kombora hilo lilinaswa kabla ya kuvuka ardhi ya Israel.
Msemaji wa kundi la Wahouthi Brigadia Jenerali Yahya Saree, amekiri kuhusika kwa kundi hilo na shambulizi hilo na kusema waliilenga kambi ya jeshi la anga ya Nevatim ya Israel kwa kile alichokitaja kuwa kombora.
Wahouthi wafyetua kombora lilolenga Kaskazini mwa Israel
Wakati huo huo, mashambulizi ya anga ya Marekani, yameendelea kuwalenga waasi hao usiku kucha, hii ikiwa sehemu ya kampeini kali ya kijeshi inayowalenga Wahouthi iliyoanza Machi 15.