MigogoroMashariki ya Kati
Israel yakosolewa katika Mkutano wa Baraza la Usalama la UN
11 Agosti 2025Matangazo
Mataifa matano ya Ulaya yalitoa tamko la pamoja katika kikao hicho maalum na kulaani uamuzi huo huku yakitoa wito kwa Israel kubadili uamuzi huo haraka. Nchi hizo zimesema hatua yoyote ya kunyakua au kukalia kimabavu ardhi ya Palestina itakuwa imekiuka sheria za kimataifa.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema mpango huo utakaoanza hivi karibuni unazilenga ngome zilizosalia za Hamas na kwamba hiyo ndio "njia bora ya kumaliza vita" akisisitiza kuwa atayafikiya malengo hayo "bila ya msaada wa yeyote. Balozi wa Palestina katika Umoja wa Mataifa Riad Mansur, ameishutumu serikali ya Israel kupuuza maoni ya Baraza la Usalama.