Israel yaunda kamati ya kushughulia uhamishaji Wagaza
25 Machi 2025Mpango huu, uliothibitishwa na maafisa wa Israeli, unafuata pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump la kuhamisha wakaazi wa Gaza, lililopingwa vikali na mataifa mengi ya Kiarabu. Ujerumani na Jordan zimeutaka mpango huo kuwa ukiukaji wa sheria za kimataifa na uhamishaji wa lazima.
Wakati huohuo, Umoja wa Mataifa umetangaza kuondoa sehemu ya wafanyakazi wake kutoka Gaza, kutokana na wasiwasi wa kiusalama baada ya shambulio dhidi ya wafanyakazi wake, huku Hamas ikitoa video inayowaonyesha mateka wawili wa Israeli inaowashikilia.
Soma pia: Zaidi ya Wapalestina 50,000 wameuawa katika vita vya Gaza
Jumuiya ya kimataifa inaendelea kuelezea wasiwasi kuhusu vurugu zinazoendelea na janga la kibinadamu Gaza, huku Umoja wa Mataifa na nchi mbalimbali wakitoa wito wa uchunguzi wa haraka na kusitishwa kwa hatua zinazoweza kuongeza mzozo zaidi.