MigogoroMashariki ya Kati
Israel yafanya mashambulizi karibu na Ikulu Damascus
2 Mei 2025Matangazo
Mashambulizi hayo yamefanyika baada ya mashambulizi mengine yanayofanana na hayo ya Alhamisi ambapo jeshi la Israel liliulenga pia mji huo mkuu wa Syria.
Soma zaidi: Israel yawashambulia wapiganaji wanaowalenga jamii ya wachache ya Druze
Hatua hizo za Israel zinafuatia shambulio baya la Jumatano huko Kusini mwa Syria lililowauwa watu 35 kutoka jamii ya walio wachache ya Druze. Vikosi vya usalama vya Syria na wanamgambo wanaoiunga mkono serikali wanatajwa kuwa ndiyo waliohusika kuwashambulia watu hao.
Soma zaidi: Israel yaishambulia mifumo ya ulinzi ya Syria
Kimsingi, watu madhehebu ya Druze wanaishi kwenye nchi za Syria, Lebanon, Israel na Jordan. Jamii hiyo inaheshimika nchini Israel na sehemu ya watu wake wanalitumikia jeshi la nchi hiyo.