Israel yafanya mashambulizi mapya mjini Damascus, Syria
16 Julai 2025Matangazo
Netanyahu amesema kuwa hali ya Sweida na kusini-magharibi mwa Syria, ni mbaya sana na kwamba jeshi la Israel na vikosi vingine vinafanya kazi kuwaokoa ndugu zao wa Druze pamoja na kuyaangamiza magenge ya utawala wa Syria.
Vikosi vya Syria vyaingia mji wa Sweida baada ya mapigano yaliyosababisha vifo
Jeshi la Israel lilishambulia karibu na lango la wizara ya ulinzi ya Syria huko Damascus na kulenga eneo hilo saa kadhaa baadaye kwa shambulizi kubwa zaidi.
Mapambano ya kimadhehebu yautikisa mkoa wa Kusini nchini Syria
Israel pia imeanzisha mfululizo wa mashambulizi ya anga kwenye misafara ya vikosi vya serikali kusini mwa Syria tangumapiganohayo yalipozuka na imeongeza wanajeshi wake kwenye eneo la mpaka.