MigogoroMashariki ya Kati
Israel kusitisha mapigano masaa 10 kwa siku huko Gaza
27 Julai 2025Matangazo
Usitishwaji huo ni kuanzia saa nne asubuhi hadi mbili usiku katika maeneo matatu yenye wakazi wengi huko Gaza ikiwa ni pamoja na Gaza City, Deir al-Balah na Muwasi.
Jeshi la Israel limesema pia kuwa limetoa misaada kadhaa huko Gaza ikijumuisha vifurushi vya unga, sukari na vyakula vya kwenye makopo, na kwamba wataruhusu uwepo wa njia salama ya kusafirisha misaada ya kibinaadamu.
Hii ni sehemu ya mfululizo wa hatua zilizochukuliwa na Israel kufuatia kuongezeka kwa wasiwasi na ukosoaji wa kimataifa kutokana na hali mbaya ya kibinaadamu inayoshuhudiwa katika Ukanda huo ikiwa ni pamoja na kuenea kwa njaa katika ardhi ya Palestina.