MigogoroMashariki ya Kati
Israel Katz: Khamenei "hawezi kuendelea kuwepo"
19 Juni 2025Matangazo
Katz ameitoa kauli hiyo wakati nchi hizo mbili zikiendelea kushambuliana vikali.
" Ningependa kusema kwamba dikteta kama Khamenei, ambaye anaiongoza nchi kama Iran, na aliyetangaza lengo baya la maangamizi ya Israel, haiwezi kuendelea kuwepo."
Katz alimlinganisha Khamenei na Kiongozi wa zamani wa manazi wa Ujerumani Adolf Hitler wakati akihutubia katika mji ulioshambuliwa wa Holon. Siku ya Alhamisi, Iran iliendesha wimbi la mashambulizi ya makombora kuelekea Israel ambapo baadhi yaliharibu vibaya hospitali ya Soroka katika mji wa jangwani wa Beersheba.