Israel haitoruhusu misaada ya kibinadamu kuingia Gaza
16 Aprili 2025Israel imesema itaendelea kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza, ambako nchi hiyo inaendeleza opresheni ya kijeshi ambayo imeligeuza eneo hilo la Wapalestina kuwa la mauaji.Soma pia:Gaza: Hospitali iliyoshambuliwa na Israel imeharibiwa vibaya
Waziri wa ulinzi wa Israel, Israel Kartz kwenye taarifa yake amesema, sera ya nchi hiyo imeweka wazi kwamba hakuna misaada ya kibinadamu itakayoingia Gaza na hatua hiyo ni moja ya kuishinikiza Hamas kutotumia fursa hiyo kama silaha.Soma pia: Hamas yatathmini pendekezo jipya la kusitisha mapigano Gaza
Israel imezuia kuingizwa kwa misaada katika Ukanda wa Gaza tangu March 2 huku mgogoro wa kibinadamu ukiongezeka kufuatia mashambulizi ya kijeshi yanayoendelea.
Watu wasiopungua 11 wameuwawa usiku wa kuamkia leo Jumatano kwa mujibu wa timu ya waokoaji.