Iran yathibitisha wafungwa walitoroka katika gereza la Evin
12 Julai 2025Matangazo
Msemaji wa idara ya mahakama Asghar Jahangir, amesema idadi ndogo ya wafungwa walifanikiwa kutoroka baada ya shambulio hilo takriban wiki tatu zilizopita, lakini hakutoa idadi kamili.
Jahangir ameendelea kusema kuwa wafungwa watano walikuwa miongoni mwa watu 71 waliouawa.
Iran: Mashambulizi ya Israel katika gereza la Evin yaliua watu 71
Israel imelitaja shambulizi hilo kama pigo la kiishara kwa serikali ya Iran.
Wanaharakati na wafungwa wa zamani wanasema shambulizi hilo lilihatarisha maisha ya wafungwa wa kisiasa.
Raia kadhaa wa Ulaya pia wamefungwa katika gereza hilo.